Aliyekuwa Naibu Rais Rigathi Gachagua amemjibu vikali Rais William Ruto, akimlaumu kwa kudunisha hadhi ya urais kwa kuzungumzia maisha ya kibinafsi badala ya masuala mazito ya kitaifa. Akizungumza makao makuu ya chama chake alipompokea Millicent Omanga, alibua madai ya ufisadi katika mradi wa Railway City jijini Nairobi.
Rigathi Gachagua, aliyekuwa Naibu Rais, alizungumza katika makao makuu ya chama chake alipompokea aliyekuwa Seneta Maalum Millicent Omanga. Alimlaumu Rais William Ruto kwa kuzungumzia maisha ya kibinafsi ya viongozi badala ya masuala kama miundombinu, usalama wa nchi na huduma za afya zinazozorota. “Huna haja ya kuzungumzia maisha ya mtu binafsi au kama ana mke au la. Unapaswa kuangazia masuala mazito kama miundombinu, usalama wa nchi na hali mbaya ya huduma za afya. Hayo ndiyo Wakenya wanataka kusikia kutoka kwa Mkuu wa Nchi,” alisema Gachagua. Kauli hiyo ilikuwa majibu ya hotuba za Ruto za hivi karibuni zinazowashambulia wakosoaji wao kuhusu maadili, mwonekano na faragha. Gachagua pia alidai ufisadi katika mradi wa Railway City. Alisema kampuni ya China Civil Engineering Construction Corporation (CCECC), iliyotoa zabuni ya chini zaidi, haikupewa kandarasi kwa kukataa kutoa hongo ya Sh7 bilioni. Badala yake, China Road and Bridge Corporation (CRBC) ilipata kandarasi kwa Sh30 bilioni, ikiongeza gharama kwa mabilioni ya pesa za walipa kodi. “Tungependa kuarifu Ubali wa Uingereza jijini Nairobi kwamba wanapaswa kufuta mradi huo na zabuni ya ujenzi wa Railway City,” alisema. Alidai kampuni zingine za China zimekataliwa kwa kukataa hongo, na Ruto ameuru CRBC pekee ipate kandarasi. Pia alimkosoa Ruto kwa kauli zake, akisema, “Sisi hatuna shida na masikio yako, tunataka yawe makubwa zaidi ili uweze kusikiliza wananchi.” Alitaja changamoto kama deni la taifa, afya na miundombinu duni.