Seneta Boni Khalwale amesajili chama kipya cha UPM ambacho kitalenga wanasiasa wa vyama vikubwa.
Seneta wa Kakamega Dkt Boni Khalwale alithibitisha katika mahojiano na Taifa Leo kuwa amesajili chama cha UPM.
Rekodi katika Afisi ya Msajili wa Vyama zinaonyesha chama hicho kimetimiza matakwa yote ya usajili.
Chama hicho kinatarajiwa kuvutia wanasiasa kutoka vyama kama ODM, DAP-K, UDA na Ford Kenya.
“UPM ni chama cha kitaifa kitakachowakusanya viongozi mashuhuri wa kisiasa nchini wanaounga mkono ajenda ya kumwondoa Rais Ruto uongozini,” alisema Khalwale.
Gavana wa Trans Nzoia George Natembeya alisema chama hicho kitazinduliwa wiki tatu zijazo na kitajumuisha viongozi wengine kama Edwin Sifuna na Godfrey Osotsi.