Aliyekuwa Rais wa LSK Faith Odhiambo amesema vuguvugu la Linda Mwananchi litageuzwa kuwa chama cha kisiasa kabla ya mwisho wa mwaka huu ili kujiandaa kwa uchaguzi wa 2027.
Odhiambo alisema maandalizi ya usajili yanaendelea ingawa chama hicho huenda kisitumie jina la Linda Mwananchi.
“Huenda chama kisitumie jina la Linda Mwananchi lakini tutakizindua mwaka huu,” alisema katika mahojiano na kituo cha televisheni Jumatatu.
Tangazo hilo lilitolewa wakati wa ziara ya viongozi wa vuguvugu hilo Kaunti ya Taita Taveta mnamo Julai 18. Mbunge wa Suba Kusini Caroli Omondi alisema uhusiano na ODM umefikia kikomo na akataka Rais William Ruto asiiingilie mchakato wa usajili.
Seneta Edwin Sifuna alidokeza kuwa anaweza kuwania urais mwaka 2027.