Kundi la Linda Mwananchi ndani ya ODM linapanga mkutano mkubwa mjini Thika mnamo Juni 14 kama sehemu ya juhudi za kujijenga kama vuguvugu la kitaifa kuelekea uchaguzi wa 2027.
Kundi hilo linalohusishwa na Seneta wa Nairobi Edwin Sifuna linaelekeza juhudi zake katika maeneo ambayo hayajawahi kuwa ngome za ODM. Hii inajiri baada ya kupata mapokezi mazuri katika eneo la Ukambani wikendi iliyopita.
Seneta wa Vihiga Godfrey Osotsi alisema lengo ni kuunganisha Wakenya kutoka maeneo yote. Alisema baada ya Thika wanapanga kuelekea Meru na Eldoret.
Mchambuzi wa siasa Dkt Joshua Wafula alisema mkutano wa Thika ni wa kimkakati kwa sababu Mlima Kenya utaendelea kuwa eneo muhimu katika uchaguzi wa urais. Kundi hilo lilitangaza mnamo Aprili mipango ya tathmini ya maeneo na kuanzisha kituo cha kuratibu shughuli zake.