Viongozi wa eneo la Pwani wakiongozwa na mawaziri na spika wa seneti wameanza mikutano ya hadhara ili kuwahamasisha wakazi kujisajili kama wapiga kura na kumuunga mkono Rais William Ruto katika uchaguzi wa 2027.
Viongozi hao wakiwemo Mawaziri Hassan Joho na Salim Mvurya pamoja na Spika wa Seneti Amason Kingi wanashirikiana na magavana wa Pwani ili kutembelea maeneo bunge yote.
Tayari wametembelea maeneo kama Likoni, Matuga, Kaloleni na Jomvu na sasa wako Mvita. Wanataka wakazi wachukue vitambulisho na kujisajili ili kutoa kura milioni nne.
Seneta Mohammed Faki alisema eneo la Pwani lina uwezo wa kutoa kura hizo lakini changamoto ni watu kutokuchukua vitambulisho. Viongozi wengine wa upinzani hawauungi mkono mpango huo.