Wadau wa sekta ya uchukuzi wamefuta mgomo uliopangwa wiki ijayo kufuatia mazungumzo na Rais William Ruto katika Ikulu ya Mombasa.
Mwenyekiti wa Chama cha Wamiliki wa Matatu, Albert Karakacha, alisema Ijumaa kuwa wadau wamekubaliana kutoendelea na mgomo huo.
“Tumefuta mgomo. Tulikuwa tumeusitisha, lakini sasa tumeufuta kabisa, kwa hivyo hatutakuwa na mgomo wiki ijayo. Tutafanya kazi,” alisema Karakacha.
Mkutano ulifanyika Alhamisi na Ijumaa, Mei 21 na 22, 2026, baada ya maandamano yaliyosababishwa na kupanda kwa bei ya mafuta. Wadau watashirikiana na serikali kwa wiki moja ili kutatua mzozo.