Mamlaka ya Kitaifa ya Usalama wa Viumbehai imewataka watafiti kuzingatia sheria za usalama wakati wa majaribio ya GMO ili kulinda afya na mazingira.
Kaimu Afisa Mkuu Mtendaji Dkt Ann Karimi alitoa wito huu wakati wa ziara ya ujumbe kutoka Senegal katika vituo vya Kalro vya Muguga na Kandara. Alisisitiza kufuata Sheria ya Usalama wa Viumbehai ya 2009 huku Kenya ikiendeleza utafiti wa bayoteknolojia.
Majaribio yanaendelea kwenye mazao kama mihogo inayostahimili magonjwa, viazi vinavyopinga late blight na mahindi ya Bt. Dkt Martin Mwirigi wa Kalro alisema lengo ni kuzalisha mazao yanayostahimili tabianchi na wadudu bila kuathiri afya ya umma.
Pamba ya Bt imekuwa ikilimwa tangu 2020 bila madhara yaliyoripotiwa. Hata hivyo kesi za kortini zinaendelea kuzuia usambazaji wa bidhaa za GMO baada ya marufuku kuondolewa mwaka 2022.