Fikirini Jacobs alifika makao makuu ya DCI Jijini Nairobi Alhamisi ili kutoa taarifa kuhusu kifo cha mwanaharakati Cecil Ouma.
Katibu wa Idara ya Masuala ya Vijana Fikirini Jacobs alisema alijibu wito wa polisi na kwamba watu saba wakiwemo walinzi wake wawili wamesha hojiwa.
Ouma alipigwa risasi Julai 1 baada ya mkutano wa vijana Kariokor. Ripoti za mashahidi zinaonyesha mgogoro ulitokea kuhusu tokeni ya pesa.
Polisi wamechukua bunduki mbili kwa ajili ya uchunguzi wa kisayansi. Familia na wakaazi wa Kariokor wanasubiri matokeo ya uchunguzi wa maiti.