Gavana wa Taita Taveta Andrew Mwadime ameomba Bunge la Taifa kutekeleza ahadi ya Rais William Ruto kuhusu kugawanya asilima 50 ya mapato ya mbuga ya Tsavo. Ahadi hiyo ilitolewa miaka mitatu iliyopita lakini bado haijatekelezwa. Mwadime alipendekeza usimamizi wa pamoja na mgawanyo wa mapato.
Licha ya kaunti ya Taita Taveta kuahidiwa na Rais William Ruto asilima 50 ya mapato ya mbuga ya Tsavo miaka mitatu iliyopita, ahadi hiyo bado haijatekelezwa. Gavana Andrew Mwadime ameomba Bunge la Taifa kutekeleza amri hiyo.
Mwadime alipendekeza sehemu ya Tsavo ibadilishwe kuwa hifadhi ya kitaifa yenye usimamizi wa pamoja na mfumo wa mgawanyo wa mapato. "Zaidi ya kilomita za mraba 10,650 za ardhi ya kaunti zimetengwa kwa ajili ya hifadhi hizo, hali inayowaacha wakazi na sehemu ndogo ya kuishi, kulima na kuendesha shughuli za kiuchumi, licha ya kaunti kubeba mzigo wa migogoro kati ya binadamu na wanyamapori ikiwa ni pamoja na uharibifu wa mazao, mifugo na hata vifo," alisema Mwadime.
Ombi hilo linatokana na wasilisho la umma kutoka kwa aliyekuwa Spika wa Bunge la Kaunti, Anselim Mwadime. Kamati ya Maombi ya Umma inatarajiwa kuchambua hoja hiyo na kuwasilisha ripoti yake kwa Bunge la Kitaifa.