Wimbi la migomo na visa vya uchomaji limepelekea kufungwa kwa shule kadhaa za upili katika kaunti mbalimbali nchini Kenya.
Zaidi ya shule 15 katika kaunti za Trans Nzoia, Nakuru, Bomet, Kericho, Narok, Kisii na Nyamira zimeathirika. Shule ya Upili ya Wasichana ya St Teresa’s Bikeke iliyoko Kiminini ilifungwa baada ya taarifa za mgomo uliopangwa.
Mkuu wa shule Eva Tsuma aliomba wanafunzi waruhusiwe kwenda nyumbani. Mkurugenzi wa Elimu Pamela Akello alithibitisha hatua hiyo huku uchunguzi ukiendelea.
Katika Nakuru, shule saba zilituma wanafunzi nyumbani ikifuatia moto uliosababisha vifo vya wanafunzi 16 mwishoni mwa Mei katika Shule ya Utumishi Girls. Mkurugenzi Victoria Mulili amesisitiza kuimarisha ushauri nasaha.
Shule zingine zilizofungwa ni pamoja na Saseta Girls, Tengecha Girls na Euro Ekulet Secondary School ambapo bweni lilichomwa.