Vurugu zimeikumba shule kadhaa nchini tangu Aprili zikisababisha uharibifu, majeraha na vifo.
Tukio la kutisha lilitokea Machi 28, 2026, katika Shule ya Upili ya Wasichana ya Utumishi, Gilgil, ambapo moto uliua wanafunzi 16 na kujeruhi wengine 79. Zaidi ya shule 18 za bweni zimeathirika katika kaunti kama Nakuru, Murang’a, Embu, Kisii, Siaya, Makueni na Pwani.
Wizara ya Elimu ilisema matukio hayo yanasababishwa na hofu ya mitihani, msongo wa mawazo na malalamishi kuhusu huduma. Katibu Profesa Julius Bitok alisema ukaguzi wa kitaifa umeagizwa ndani ya wiki mbili na idadi ya maafisa wa ubora imeongezwa hadi 1,000.
Mwenyekiti wa Chama cha Wazazi Silas Obuhatsa alisema hali ni ya dharura ya kitaifa na sio matukio ya pekee. Alitoa wito wa kutekeleza sera za usalama shuleni kikamilifu.