Shirika la Hali ya Hewa Duniani limetangaza uwezekano wa asilimia 90 wa El Niño kujitokeza nusu ya pili ya mwaka huu na kuathiri Kenya.
Jumanne Shirika la Hali ya Hewa Duniani lilitangaza kuwa kuna uwezekano wa asilimia 90 kwamba El Niño itajitokeza katika nusu ya pili ya mwaka huu. Katibu Mkuu wa shirika hilo Celeste Saulo alisema dunia inapaswa kujiandaa kwa El Niño yenye nguvu ambayo inaweza kuongeza ukame mvua kubwa na mawimbi ya joto.
El Niño ya 2023-2024 ilikuwa miongoni mwa tano zenye nguvu zaidi kuwahi kurekodiwa duniani na ilichangia viwango vya juu vya joto mwaka 2024. Nchini Kenya wataalamu wanatarajia mvua za wastani hadi chini ya wastani katika miezi ya Juni Julai na Agosti hasa katika maeneo ya magharibi na bonde la ufa.
Wakati huo huo joto la juu kuliko kawaida linatarajiwa kushuhudiwa kote nchini. Mwanasayansi wa hali ya hewa Dkt Chris Kiptum amesema mvua nyingi inatarajiwa mwishoni mwa mwaka na inaweza kusababisha mafuriko katika maeneo ya mijini.
Wataalamu wanaonya kuwa athari zitategemea pia hali ya Indian Ocean Dipole na wanahimiza maandalizi mapema ili kupunguza madhara.