Wadau wa sekta ya uchapishaji nchini Kenya wameitaka serikali kuimarisha sheria dhidi ya wizi wa vitabu ili kuwalinda waandishi na tasnia ya fasihi.
Chama cha Wachapishaji Vitabu Kenya kilisema uchapishaji haramu unasababisha hasara ya zaidi ya shilingi bilioni tatu kila mwaka.
Wadau hao walizungumza wakati wa hafla ya pili ya Tuzo za TBC Penmanship iliyofanyika katika ukumbi wa Jain Bhavan Auditorium, Loresho, Nairobi.
Afisa Mkuu Mtendaji wa Text Book Centre, Sachin Varma, alisema tuzo hizo zinawapa waandishi chipukizi nafasi ya kuonyesha vipaji vyao.
Miongoni mwa washindi ni Janet Mbugua kwa kitabu My First Time, Dkt Anuradha Khoda kwa Noah and the Rainbow Promise Series 2 na Jackson Biko kwa Big Little Fights.