Waziri wa Utumishi wa Umma Geoffrey Ruku alishangaa wakati wa ziara yake Garissa Alhamisi asubuhi alipokuta afisi nyingi za serikali zimefungwa na watumishi hawapo kazini.
Waziri Ruku alifika Garissa usiku wa kuamkia Alhamisi na kufika afisini asubuhi. Alikuta jengo lote likiwa na afisa mmoja tu na milango mingi imefungwa.
Alisema afisi zinapaswa kufunguliwa saa moja na nusu asubuhi kulingana na mwongozo wa 2016 wa eneo la Kaskazini Mashariki. Mapumziko ya saa mbili yanaruhusiwa wakati wa mchana ili kuruhusu Waislamu kuswali.
Kamishna wa Kanda ya Kaskazini Mashariki John Otieno hakuwepo kwani alikuwa Wajir akisimamia maandalizi ya sherehe za Madaraka Day zitakazofanyika Juni 1, 2026.
Waziri alisisitiza kuwa watumishi wanapaswa kuwa makini baada ya serikali kuongeza mishahara yao kuanzia Julai 1, 2025.