Mahakama ya Rufaa imeondoa agizo lililozuia utekelezaji wa mkataba wa afya wa dola bilioni 1.6 kati ya Kenya na Marekani uliotiwa saini Desemba 2025.
Jopo la majaji watatu liliondoa zuio hilo lililokuwa limesimamisha makubaliano hayo hadi kesi itakaposikizwa Oktoba 30, 2026. Mwanasheria Mkuu Dorcas Oduor na Wizara ya Afya walisema kusimamishwa kulisababisha pengo kubwa katika sekta ya afya wakati magonjwa kama Ukimwi, kifua kikuu na malaria yanaongezeka.
Serikali ilieleza kuwa mfumo huo utasaidia kununua vifaa vya matibabu, kuongeza dawa, kuajiri wahudumu na kupanua huduma za bima. Marekani imejitolea kutoa fedha hizo kwa miaka mitano.
Seneta Okiya Omtatah na Shirika la watumiaji nchini (COFEK) walipinga mkataba huo wakidai ulikiuka Katiba na kuwa na hatari ya data za afya kuvuja. Serikali ilihakikisha kuwa taarifa zitakazotolewa ni za jumla tu na haziwezi kumtambulisha mtu binafsi.