Waziri wa Kilimo Mutahi Kagwe amewahakikishia wakulima wa majanichai kuwa ushuru mpya wa asilimia 0.8 hautapunguza mapato yao.
Waziri Kagwe alisema ushuru huo unaolengwa na Bodi ya Majanichai Kenya utalipwa na wauzaji wa nje pekee. Aliongeza kuwa asilimia 50 ya mapato yatakayokusanywa yatatumika kulinda na kuboresha mapato ya wakulima.
Ushuru wa asilimia 0.8 utatozwa kwenye mauzo ya chai kupitia mnada au moja kwa moja nje ya nchi. Wakati huo huo waagizaji kutoka nje watalipa asilimia 100 ya thamani ya chai iliyosindikwa ili kulinda wakulima wa ndani.
Wakulima wadogo, vyama vya ushirika na watumiaji wa ndani hawataathirika na ushuru huo. Inatarajiwa kukusanya Sh1.42 bilioni kwa mwaka kutokana na mauzo ya nje na uagizaji.